Free Web Hosting by Netfirms
Web Hosting by Netfirms | Free Domain Names by Netfirms


Gazeti INJILI
Kwenye Internet
http://munishi.com

Tel. 254722602445 E-mail: munishifaustin@yahoo.com
Or fmunishi@hotmail.com

Serikali Yatatiza usafiri Kenya


Kufuatia agizo la serikali kwamba matatu zote ziwekwe vithibiti mwendo pamoja na mikanda, maelfu wamekosa usafiri kwenda kwenye sehemu zao za kazi. Pamoja na kwamba matatu nyingi hazijatimiza agizo la serikali, tuna mashaka kwamba hata kama zote zitatimiza agizo hilo, matatizo ya usafiri bado yatakuwa mbali na kumalizika. Pamoja na kujaza abiria kupindukia, bado matatu zilikuwa hazikithi mahitaji ya usafiri sawa sawa. Tunaiunga mkono hatua ya serikali kushurutisha nidhamu katika sekta ya usafiri, lakini sambamba na hilo tunaitaka ichukue hatua zaidi. Hii itakuwa ni pamoja na kutengeneza barabara zilizopo pamoja na kuongeza nyingine mpya. Tena usafiri wa reli uimarishwe na ikiwezekana zijengwe reli za chini ya ardhi mijini na za kwenda mikoani. Serikali wangeanza na hilo, hili la sasa lingekuwa rahisi kutekelezeka.

ILa mambo yalivyo sasa ni kwamba abiria waliotarajiwa kusaidiwa, ndio wanaoteseka na hata kuweka maisha yao hatarini zaidi. Wengi wamekosa nafasi katika matatu chache zilizotimiza agizo la serikali, na matokeo ni kupanda malori au Pick ups ambazo hazina mikanda wala vithibiti mwendo. Taxi nazo zimepata biashara kubwa ya kubeba abiria. Zenyewe hazina vithibiti mwendo wala mikanda ya kufunga. Kutokana na wingi wa abiria, nao itawabidi wakimbie mwendo wa kasi kuwahi abiria. watafanya kile kilichokuwa kinawaponza madereva wa matatu. Tamaa ya pesa. Hali kama hiyo inapotokea, abiria aliyetarajiwa kulindwa na ajali barabarani anajikuta akiwa hatarini kuliko mwanzo.

Hatuipingi hatua ya serikali, lakini utekelezaji wake lazima uwe wa muda mrefu. Vinginevyo itakuwa sawa na kuruka majivu na kukanyaga moto. Matatu kama zilivyo biashara nyingine, wanataka wapate faida ili waweze kuwalipa madereva na wasaidizi wao. Inapokuwa safari ya saa moja inabidi ichukue masaa mawili hii itapunguza wingi wa safari kwa siku. Sambamba na hilo abiria waliokuwa wakijazana sasa hawatakuwepo. Ukizingatia yote hayo wenye matatu wataachwa na suluhu moja tu. Nayo ni kuongeza nauli. Siyo kwamba wataongeza, tayari wameshaongeza. Mahali pa shilingi arobaini sasa abiria wanalipa mia moja. Wakilalamika wanaulizwa kwamba "huoni umekaa raha mustarehe kuliko mwenye gari ya binafsi? Umejifunga mkanda, unasoma gazeti, kama husomi gazeti umelala usingizi, raha zote hizo hutaki kuzilipia? Hata kama ni gari yako binafsi ingebidi umwajiri dereva ndipo uweze kustarehe kama unavyostarehe hapa kwenye matatu. Na hapo hatujazungumza kuhusu petroli kila siku na matengenezo ya gari yako. Kwa hiyo wacheni maneno mengi, ongezeni nauli." Hayo ndiyo maneno ambayo abiria watakutana nayo kila watakaposafiri.

Siyo kwamba matatizo ya usafiri yatawaadhiri abiria peke yao, la hasha. Hata serikali itaadhirika kwani wengi watashindwa kuwasili katika sehemu zao za kazi mapema, na hii itaharibu uchumi zaidi. Je hilo ndilo lengo la serikali? Kama jibu lake ni hapana, basi lazima marekebisho ya sekta zote yafanywe kwa makini zaidi ili wale waliotarajiwa kusaidika na marekebisho hayo wasiwe ndio wanaoumizwa nayo.

Kuna mengi yanayofanywa kwa nia nzuri lakini yanageuka kuwa kero kwa wananchi. Kwa mfano majumba yanayotarajiwa kubomolewa kwa madai kwamba yamejengwa barabarani. Itaeleweka na kuingia akilini zaidi wakati ujenzi wa barabara husika utaonekana kukwamishwa na nyumba iliyojengwa kwenye mkondo wa barabara. Nyumba kama hiyo ikibomolewa itaeleweka lakini baada ya serikali kuwafidia wenye nyumba hizo. Hawa wenye nyumba hizo bado ni wananchi waaminifu kwa serikali hii mpya kama walivyokuwa waaminifu kwa serikali ya zamani iliyowamilikisha maeneo kimakosa. Ilikuwa nje ya uwezo wao kuirekebisha serikali ya awali, na hata sasa ni nje ya uwezo wao kuipinga hatua ya serikali iliyoko madarakani kubomoa nyumba zao, Pia itakuwa nje ya uwezo wao wakati serikali ijayo itakapowaruhusu wengine wajenge kwenye maeneo kama hayo. Tunayosema hapa ni kwamba serikali isiwaadhibu wananchi kwa makosa ya serikali ya awali. Serikali ya sasa inatakiwa kuiadhibu serikali ya awali na siyo wananchi. Sisi wananchi tunaiona serikali mpya kama mkombozi wetu. Ikiwa MKOMBOZI atatenda mambo yatakayowaumiza waliotarajia kukombolewa, uchungu wake utakuwa mara dufu.

Kabla ya agizo la serikali, mambo yalikuwa hivi:


Tangaza Biashara yako Bure
Tuma picha na maelezo kwa munishi@munishi.com

http://munishi.com FREE!
Send a photo and information to munishi@munishi.com

Bonyeza HAPA kwa picha zaidi 2 3 4

 

Biblia Inasemaje? Ukimwi Unaua Jiadhari- KENEDY Wewe Unasemaje? Mwinyi Aliibadili Tanzania Wewe Unasemaje? Nation TV Yakosa Mwelekeo Wewe Unasemaje? Siasa na Dini Zitenganishwe? Kweli serikali haina dini? Wewe Unasemaje? Waislam Wampora Mkisto Nyumba Wewe Unasemaje? Nyerere Msingi aloujenga Haufai Tuubomoe? Wewe Unasemaje? Mjue Kaka Paul Wewe Unasemaje? "Nisaidieni Nioe" Asema Jeff WACIAMAWewe Unasemaje? Mkapa Hatoki Muda Ukiisha Wewe Unasemaje? Marandu T.L Ajitoa Kwenye "FORUM"Kisha Akarudi TenaWewe Unasemaje?MUNISHI AZINDUA HERALD Wewe Unasemaje? Majira Wajaribu Kumzima Munishi? Wewe Unasemaje? Professor Oloo Amlaumu Mwinyi Wewe Unasemaje? Taliban Wamefanya Kiungu, Amerika walifanya kishetani Wewe Unasemaje? Philip Ochieng attacks Mkapa- Wewe Unasemaje?Moi Aombewa Amalize Vizuri Wewe Unasemaje?Rodnat Mwenda Amshambulia MunishiWewe Unasemaje? SIKU TATU BAADAYE Majambazi Wamvamia Munishi NyumbaniWewe Unasemaje? NYERERE ALISHINDWA MENGIWewe Unasemaje? Leila Asema Alikuwa ShujaaWewe Unasemaje? Wengi Wampinga Leila Wewe Unasemaje? EAGT Dodoma kunafuka Moshi Wewe Unasemaje? ASKOFU KULOLA AMTIMUA MCHUNGAJI ARUSHA Wewe Unasemaje? Mwazembe Amtetea Kulola NAYE MWAKIPESILE ASEMA EAGT IMEOZA Wewe Unasemaje? Kwa Nini Waislamu Wanalalamika? KITABU HIKI MARUFUKU TANZANIA Wewe Unasemaje? Hofu ya Mabomu Imetanda Dar es Salaam SERIKALI YALAUMIWA KUWANYANYASA WAISLAMU Wewe Unasemaje? Amerika Siyo Mungu WENGI WASEMA IJILAUMU YENYEWE. ISIPOBADILI SERA MAMBO BADO Gazeti la Nation Lasema Kenya Ilikosea Kutangaza Msimamo Haraka. Wewe Unasemaje? NALO GAZETI LA An-Nuur Lamwita Osama Shujaa Na Mpigania Haki Wewe Unasemaje? YESU NI MUNGU? Wewe Unasemaje? Haki za Wanaume Wewe Unasemaje? POLISI TANZANIA WALIUA ZAIDI YA70 HUKO ZANZIBAR Serikali Ilihusika Na Mauaji Ya Raia Wasio Na Hatia Wewe Unasemaje? CCM ILIWAITA WALIOUAWA MAGHAIDI Wewe Unasemaje? Serikali Inayoua Raia Haifai WENGI WANAOMBA MUNGU AIANGUSHE CCM Wewe Unasemaje? Mkapa Asema Nguvu Za Dola Zitamshinda Mungu Wewe Unasemaje? Waziri wa Viwanda TZ Amejiuzulu Wewe Unasemaje? WorldSpace Hawajui Wamlenge Nani Wewe Unasemaje? Dani Hagael Amsaga Askofu Habari Katika Picha Wewe Unasemaje? Mrema Awapongeza Afghanistan Wewe Unasemaje? CUF Kujitoa katika muafaka-Wewe Unasemaje? Gospel tape banned by Dar officials Wewe Unasemaje? Bonyeza kichwa cha habari kusoma Habari, au bonyeza "Wewe Unasemaje?" kutoa maoni yako. Kumbuka! maoni yako yatachapishwa hapo kwa hapo kwenye mtandao, na yatasomwa duniani kote sasa hivi.Tembelea Web Site zetu mpya kwa habari zaidi: http://ktn2.netfirms.com http://nipashe.netfirms.com munishifaustin.netfirms.com http://nation.netfirms.com http://munishi.topcities.com

Faustin Munishi Tell. 25472602445 Nairobi Kenya East Africa
E-mail: fmunishi@hotmail.com  |  munishifaustin@yahoo.com

Check mail at Hotmail
Check Mail at Yahoo